Rais Donald Trump aishambulia tume maalum ya uchunguzi inayoongozwa na Robert Mueller. Uingereza bado yaikalia kooni Urusi juu ya matumizi ya sumu. Na Waziri wa mambo ya ndani wa Ujerumani Horst Seehofer, ameutuhumu Umoja wa Ulaya kwa kuchukuwa msimamo wa kibabe kuhusu ugawaji wa wahamiaji.