1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mapigano yazuka tena Sudan

22 Aprili 2023

Mapigano kati ya makundi hasimu ya kijeshi nchini Sudan yaliendelea usiku kucha baada ya kile kinachoelezwa kusitisha mapigano kwa muda mfupi kupisha sherehe za Eid al-Fitr

https://p.dw.com/p/4QR8X
Konflikt im Sudan
Picha: Maheen S/AP/dpa

Mwandishi wa habari wa Shirika la Habari la Ujerumani DPA katika eneo la tukio amesema katika mji mkuu wa Khartoum kumetokea miripuko mingine ya mabomu, huku mashuhuda wengine wakiandika katika kurasa zao za Twittr kusikika kwa milio ya risasi.

Mwandishi DPA alisema usitishwaji  mapigano uliokuwa na lengo la kutoa nafasi ya sherehe za Eid al-Fitr kwa kuadhimisha mwisho Mwezi mtukufu wa Ramadhani, kwa kiasi kikubwa ulifanyika wakati wa usiku ingawa pia kulikuwa na kile alichosema mapigano ya hapa na pale.

Mapigano nchini Sudan yalizuka takribani juma moja lililopita kati ya majenerali wawili wenye nguvu zaidi na vitengo vyao vya kijeshi. Kiongozi wa kijeshi Abdel Fattah al-Burhan, ambaye pia ni kamanda mkuu wa jeshi, anakabliana na naibu wake Mohammed Hamdan Dagalo, kiongozi kikundi chnye nguvu cha kijeshi cha RSF.