1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa kilele Ulaya na Arabuni

4 Machi 2019

Kwa nini ilichukuwa muda mrefu hivi kwa mahusiano ya pande hizi mbili kuonekana muhimu kwa kiwango hiki cha ngazi za juu? Kipi kinachowakutanisha leo na ambacho hakikuwepo kabla? Yapi mapungufu ya kimahusiano baina yao na vipi namna ya kuyarekebisha?  

https://p.dw.com/p/3EOnR

Wiki iliyopita ulimalizika kwa mkutano wa kilele kati ya Umoja wa Ulaya na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu uliofanyika Sharm Al Shaikh, nchini Misri. Huu ulikuwa mkutano wa kwanza kabisa wa aina yake baina ya pande hizi mbili, ambazo sio tu  kwamba zinapakana kijiografia, lakini pia zina historia inayogusana kupitia ukoloni na wakati mwengine hata siasa za kilimwengu.

Pande zote mbili kwenye mkutano huo zilikiri kwamba mkutano huu ulikuwa umechelewa sana na kwamba lazima uendelee kuwapo mlahaka baina ya vyombo viwili hivi, huku pakipangwa mwaka 2022 kuwa ni mwaka wa kukutana tena mjini Brussels, Ubelgiji.

Washiriki kwenye mjadala huu ni mchambuzi wa masuala ya kimataifa, Ahmed Rajab, akiwa London, Uingereza. Mtaalamu wa siasa za Mashariki ya Kati, Dk. Harith Ghassany, akiwa Muscat, Oman na mwandishi wa habari na mchambuzi wa masuala ya Ghuba, Abdulfattah Mussa.