1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Urusi yaishtumu Ukraine kwa shambulizi

1 Agosti 2023

Mamlaka nchini Urusi mapema leo kwa mara nyengine zimeishutumu Ukraine kwa shambulizi jengine la ndege zisizokuwa na rubani katika ardhi yake.

https://p.dw.com/p/4UdKF
Rais wa Urusi Vladmir Putin
Rais wa Urusi Vladmir PutinPicha: Sergei Bobylev/TASS/imago imagesTASS

Urusi inasema mojawapo ya droni hizo zimelenga jengo katika mji mkuu ambalo lilikuwa limeharibiwa na droni nyengine siku chache tu zilizopita katika shambulizi sawa na hilo. Wizara ya mambo ya nje ya Urusi imesema mapema leo kwamba imezidungua ndege mbili zisizo na rubani nje ya Moscow.

Urusi yasema Ukraine yaonesha kushindwa kulipiza kisasi

Maafisa wa Urusi wamedai hatua ya Ukraine kuzidisha mashambulizi mjini Moscow inaonesha kushindwa kwake katika kulipiza kisasi. Mwishoni mwa wiki iliyopita, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy alisema kwamba, "vita taratibu vinarudi ndani ya Urusi" ingawa hakukiri kuhusika kwa majeshi yake na shambulizi la droni siku ya Jumapili.