1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMali

Mali wapigia kura rasimu mpya ya katiba

18 Juni 2023

Raia nchini Mali wanaipigia kura rasimu ya katiba mpya ambayo inakusudia kufungua njia ya uchaguzi wa kidemokrasia.

https://p.dw.com/p/4SjYn
Mali Bamako | Abstimmung über Verfassungsänderung
Picha: Fatoma Coulibaly/REUTERS

Utawala wa kijeshi nchini humo umesema kura hiyo inaanzisha mchakato wa mpito wa kurejeshwa kwa utawala wa kiraia. Uchaguzi wa bunge umepangwa kufanyika mwezi Oktoba na ule wa urais utafanyika mwezi Februari.

Hata hivyo kura ya leo ya kuamua juu ya katiba mpya ilicheleweshwa kwa miezi mitatu huku wasiwasi ukisalia bado, ikiwa utawala wa kijeshi utaheshimu mchakato huo.

Chini ya katiba mpya inayopendekezwa itakayochukua nafasi ya katiba ya mwaka 1992, jukumu la rais na jeshi vitapewa mamlaka makubwa kupitia bunge.