1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mahakama ya kijeshi Misri yawahukumu kifo watu 17

Oumilkheir Hamidou
11 Oktoba 2018

Watu 17 wamehukumiwa kifo na mahakama ya kijeshi Misri kwa kuhusishwa na mashambulizi kadhaa ya mabomu katika makanisa

https://p.dw.com/p/36NH5
Ägypten Anschlag
Picha: Picture-alliance/AP/A. Hatem

Mahakama ya kijeshi ya Misri imewahukumu kifo watu 17 leo kuhusiana na mashambulio kadhaa ya mabomu ya kujitoa muhanga  katika makanisa. 

Kundi la Dola la Kiislamu lilidai kuhusika na mashambulizi hayo ambayo yalisababisha watu kadhaa kufariki.

Watu wengine 19 wamehukumiwa kifungo cha maisha na wengine 10 wamehukumiwa kifungo  cha  miaka  kuanzia  10  hadi  15.

Watu 74 waliuwawa  katika  mashambulizi mwaka 2016  na 2017 mjini  Cairo, Alexandria na mji  ulioko ukingoni mwa mto Nile wa  Tanta. Waliolengwa ni Wakristo wa madhehebu ya Coptic, ambao  ni asilimia 10 ya wakaazi wa Misri ambao wakaazi wake wengi ni  Waislamu  wa  madhehebu  ya Sunni.

Tangu kuondolewa madarakani kwa kiongozi mfuasi wa nadharia za Kiislamu Mohammed Mursi mwaka  2013, mamia ya polisi , wanajeshi na raia wameuwawa katika mashambulizi ya wapiganaji wa jihadi.