1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Mahakama Israel yataka wafanyakazi kusitisha mgomo mara moja

2 Septemba 2024

Mahakama ya kazi nchini Israel imeagiza kusimamishwa kwa mgomo wa nchi nzima ulioitishwa na chama cha wafanyakazi, wanaoishinikiza serikali kufikia makubaliano ya kuachiliwa mateka wanaoshikiliwa Gaza.

https://p.dw.com/p/4kCBC
Maandamano ya kupinga serikali ya Israel Tel Aviv
Maelfu ya raia wakiandamana mjini Tel Aviv kuishinikiza serikali ya Waziri Mkuu Netanyahu kukubali kusitisha vita ili kurejeshwa kwa wapendwa wao wanaoshikiliwa mateka na HamasPicha: Jack GUEZ/AFP

Mahakama ya kazi nchini Israel imeagiza kusimamishwa kwa mgomo wa nchi nzima ulioitishwa na chama cha wafanyakazi, wanaoishinikiza serikali kufikia makubaliano ya kuachiliwa mateka wanaoshikiliwa Gaza.

Hukumu ya mahakama hiyo ya Tel Aviv aidha imesema mgomo huo umechochewa kisiasa.

Somam pia:Waisraeli waanzisha mgomo wakishinikiza kuachiliwa kwa mateka

Hukumu hiyo imetolewa baada ya Waziri wa Fedha Bezalel Smotrich anayepinga makubaliano katika vita kati yao na Hamas, kuiomba mahakama kuuzuia mgomo huo.

Mahakama hiyo imesema mgomo huo haukuitishwa kwa sababu za kiuchumi, na shirikisho hilo linaruhusiwa kuitisha migomo kwa sababu za kiuchumi na haki za wafanyakazi na si za kisiasa.