1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiUfaransa

Rais Macron kukutana na mameya wiki hii kufuatia vurugu

3 Julai 2023

Kulikuwa na vurugu za hapa na pake nchini Ufaransa usiku wa kuamkia leo lakini pia dalili kuwa maandamano yenye ghasia ambayo yameikumba nchi hiyo kwa siku kadhaa yanapungua.

https://p.dw.com/p/4TLIX
Frankreich | Proteste und Ausschreitungen nach dem Tod eines 17-jährigen
Picha: Alexandre Marchi/MAXPPP/dpa/picture alliance

Wizara ya mambo ya ndani imesema ni watu 49 pekee waliokamatwa kufikia usiku wa manane, ikiwa ni idadi ndogo zaidi ikilinganishwa na siku zilizopita.

Ghasia zilizuka katika baadhi ya miji kama vile Lyon, ambako polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya wanaharakati wa misimamo mikali ya mrengo wa kulia.

Rais Emmanuel Macron anapanga kukutana kesho na zaidi ya mameya 200 ambao maeneo yao yaliathirika na maandamano hayo ya kitaifa.

Macron pia atakutana leo na marais wa Seneti na Bunge. Jana usiku alifanya mkutano wa dharura na mawaziri wake.

Soma pia: Polisi nchini Ufaransa yawakamata zaidi ya watu 719 wakati wa ghasia za kupinga ukatili wa polisi

Ufaransa imekumbwa na vurugu na uporaji kufuatia kuuliwa kwa kupigwa risasi kijana mwenye umri wa miaka 17 na polisi wa barabarani viungani mwa mji mkuu Paris.

Bibi ya kijana huyo ametoa wito kwa waandamanaji kusitisha vurugu zao.