1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Macron kwenda China kujadili vita vya Urusi na Ukraine

25 Februari 2023

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema ataitembelea China mapema mwezi Aprili, huku akiitolea mwito nchi hiyo kusaidia kuishinikiza Urusi kusitisha vita vyake Ukraine.

https://p.dw.com/p/4NylH
Frankreich Deutschland China Ukraine Russland Macron Scholz Xi
Picha: Benoit Tessier/AP Photo/picture alliance

Akizungumza siku moja baada ya China kuomba mazungumzo ya amani kufanyika kati ya pande hasimu huku ikitangaza mipango yake ya kumaliza vita hivyo, Macron amesema amani itapatikana iwapo Urusi itasitisha uchokozi wake, kuondoa wanajeshi wake na kuheshimu uhuru wa Ukraine pamoja na watu wake. 

Wafadhili wakutana Paris kusaidia Ukraine

Ameitahadharisha China kutotoa silaha kwa Urusi na kuitaka pia Beijing kuiomba Moscow kutothubutu kutumia silaha za sumu au nyuklia dhidi ya Ukraine. 

China ilitoa pendekezo la vipengele 12 la kutafuta suluhu ya kisiasa katika vita vya Urusi na Ukraine, baada ya madai kutoka kwa nchi za Magharibi kwamba, China inafikiria kuipa silaha Urusi madai ambayo imeyakanusha.