1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

Maandamano ya wakulima yasambaa Ulaya kabla ya mkutano wa EU

31 Januari 2024

Wakulima wa Ufaransa na Ubelgiji waliokasirishwa na kupanda kwa gharama, sera za mazingira za Umoja wa Ulaya na uagizaji wa chakula cha bei nafuu walifunga barabara kuu na barabara za kuingia katika bandari.

https://p.dw.com/p/4brSN
Maandamano ya wakuliwa wa Ufaransa
Maandamano ya wakuliwa wa UfaransaPicha: BERTRAND GUAY/AFP

Nchini Ubelgiji, wakulima walifunga barabara zinazoelekea bandari ya shehena ya Zeebrugge ambayo ni ya pili kwa ukubwa nchini humo.

Walisema wanalenga kuzruia barabara za kuingia katika bandari hiyo kwa saa 36 kwa sababu wanasema inapokea msaada wa kiuchumi badala ya wakulima.

Maandamano hayo yameongeza kasi kabla ya kufanyika mkutano wa kilele wa Umoja wa Ulaya kesho Alhamisi.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema atalijadili suala hilo na rais wa Halmashauri Kuu ya Ulaya Ursula von der Leyen na viongozi wa serikali za umoja huo.

Maandamano hayo yanafuatia mengine sawa na hayo yaliyofanywa na wakulima karibu kote barani Ulaya ikiwemo nchini Ujerumani, Poland na Romania.