1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maandamano ya uhamiaji yavuruga bandari ya Rhodes

Hawa Bihoga
29 Oktoba 2023

Takriban wahamiaji na wakimbizi 400 wamefanya maandamano Jumapili katika bandari ya kisiwa cha Rhodes, wakishinikiza kuhamishiwa katika maeneo mengine nchini Ugiriki na kutatiza usafiri bandarini hapo

https://p.dw.com/p/4YAas
Wahamiaji na wakimbizi wengi huwasili katika kisiwa cha Lampedusa
Wahamiaji na wakimbizi wengi huwasili katika kisiwa cha LampedusaPicha: Zakaria Abdelkafi/AFP

Takriban wahamiaji na wakimbizi 400 wamefanya maandamano leo Jumapili katika bandari ya kisiwa cha Rhodes, wakishinikiza kuhamishiwa katika maeneo mengine nchini Ugiriki na kutatiza usafiri bandarini hapo.

Soma pia: Zaidi ya wahamiaji 1,400 wa Kiafrika wawasili visiwa vya Canary

Wengi wa waandamanaji hao waliokuwa wakipinga hali zao duni, ni wale waliookolewa baada ya kuvuka bahari hatari ya Mediterania kisha kusafirishwa hadi katika kisiwa hicho kwa ajili ya kushughulikiwa maombi yao ya ukimbizi. Mazungumzo yanaendelea kati ya wahamiaji hao na idara ya polisi kisiwani humo.

Kwa mujibu wa takwimu rasmi wahamiaji na wakimbizi 10,790 waliwalisili Ugiriki katika miezi minane ya kwanza 2023, hii ikiwa ni mara dufu ya takwimu za mwaka uliopita ambapo takriban watu 5,216 waliingia nchini humo.