1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LAGOS: Marekani na Uingereza zafunga ofisi zake za ubalozi NIgeria

17 Juni 2005
https://p.dw.com/p/CF2d

Marekani imefunga ubalozi wake mjini Abuja na ubalozi wake mdogo mjini Lagos kufuatia kile ilichokiita ukosefu wa usalama. Lakini kwa mujibu

wa msemaji wa Ubalozi huo hana taarifa zozote kuhusiana na tukio lolote la kiusalama.

Polisi wa Nigeria wanachunguza madai hayo.

Kufuatia hatua hiyo ya Marekani Uingereza pia imefunga Ubalozi wake mjini Lagos kufuatia wasiwasi huo.

Duru za kidiplomasia nchini humo zimesema kwamba Marekani imepokea vitisho kutoka kwa wapiganaji wa kigeni walioko nchini Nigeria.

Hata hivyo wanadiplomasia na wachunguzi wanasema hakuna ushahidi wowote hadi sasa wa kuonyesha kundi linaloongozwa na Osama Bin Laden la Alqaeda lipo nchini humo.