1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LAGOS: Machafuko mapya yazuka Nigeria

11 Julai 2006
https://p.dw.com/p/CG8Z

Si chini ya watu 8 wameuawa na wengi wengine wamejeruhiwa katika mapambano yaliyozuka upya kati ya vikosi vya usalama na makundi ya waasi katika mji wa Onitsha,kusini-mashariki mwa Nigeria.Mapambano hayo yalizuka baada ya vikosi vya polisi kujaribu kuyafukuza makundi hayo kutoka mji huo.