Nchini Tanzania kumekuwa na mjadala mkali haswa katika mitandao ya kijami kuhusiana na kile kinachotajwa kuwa kuzuka kwa mafua makali nchini humo. Licha ya mjadala huo kuonekana kudhihirisha wasiwasi unaowakumba wananchi, serikali haijatoa tamko au taarifa rasmi juu yake. Mwandishi wa kanda ya ziwa Dotto Bulendu ametujulisha kinachoendelea.