Kremlin yasema Putin yupo imara
27 Juni 2023Matangazo
Msemaji wa Ikulu ya Kremlin, Dmitry Peskov, amesema uasi huo uliozimwa badala yake umeonesha jinsi jamii ya Kirusi ilivyoshikamana na rais Putin hata katika nyakati za mashaka.
Wakati huo huo, Rais Putin amewahutubia wanajeshi wa nchi yake na kuwasifu kwa kuzuia kile alichosema ni "vita vya wenyewe kwa wenyewe" ambavyo vingetokea kutokana na uasi wa kundi la Wagner.
Kwenye hotuba yake, Putin pia amekiri kwa mara ya kwanza kwamba Moscow imekuwa ikilipatia fedha kundi la Wagner licha ya hapo kabla Urusi kukanusha kuwa haina mafungamano la kundi hilo.