Ambapo si rahisi kuwa na wachapishaji wa kazi za fasihi hasa katika mataifa masikini, nchini Tanzania waandishi wa riwaya za Kiswahili wamegundua njia ya kuhakikisha kuwa kazi zao zinasomwa na hadhira yao kwa kuanzisha chama cha kuwachapishia na kuwauzia riwaya hizo kinachoitwa UWARIDI. Profesa Uta Reuster wa Chuo Kikuu cha Hamburg, Ujerumani, amefanya utafiti kuhusiana na juhudi hizi.