1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kiongozi wa Iran afungua mlango wa mazungumzo ya Nyuklia

27 Agosti 2024

Kiongozi mkuu mwenye mamlaka makubwa zaidi nchini Iran Ayatollah Ali Khamenei, amefungua mlango wa kukaribisha kuanzishwa tena mazungumzo na Marekani juu ya mpango wake wa Nyuklia.

https://p.dw.com/p/4jyaO
Kiongozi mkuu nchini Iran Ayatollah Ali Khamenei
Kiongozi mkuu nchini Iran Ayatollah Ali KhameneiPicha: Iranien Supreme Leader/ZUMA Wire/IMAGO

Kiongozi mkuu mwenye mamlaka makubwa zaidi nchini Iran Ayatollah Ali Khamenei, amefungua mlango wa kukaribisha kuanzishwa tena mazungumzo na Marekani juu ya mpango wake wa Nyuklia.

Khamenei ameiambia serikali ya nchi yake kwamba hakuna kinachowazuia kufanya mazungumzo na adui. Kauli hiyo ya Khamenei  inaonesha kufunguwa njia ya kukaribisha mazungumzo yoyote yatakayofanyika chini ya serikali inayoongozwa na rais mwanamageuzi Masoud Pezeshkian.

Hata hivyo Khamenei mwenye umri wa miaka 85, ambaye ana maamuzi ya mwisho kuhusu sera  za Iran, amemtahadharisha Pezeshkian na serikali yake kutambuwa  kwamba Marekani sio nchi ya kuaminiwa.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW