1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kim Jong Un akutana na rais Vladmir Putin nchini Urusi

13 Septemba 2023

Rais wa Urusi Vladmir Putin amesema atajadili masuala mbali mbali na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un ambaye yuko ziarani nchini humo.

https://p.dw.com/p/4WHTS
Russland | Treffen Kim Jong Un und Wladimir Putin
Picha: Vladimir Smirnov, Sputnik, Kremlin Pool Photo via AP/picture alliance

Kim Jong Un ameahidi ushirikiano wa karibu zaidi na Moscow akisema nchi yake iliyotengwa kimataifa siku zote itakuwa pamoja na Urusi.

Picha zilizotolewa na ikulu ya Urusi zimewaonyesha viongozi hao wawili wakisalimiana katika kituo cha safari za anga za mbali cha  Vostochny Cosmodrome. Rais Putin amesema eneo hilo la mkutano limechaguliwa mahususi kwa sababu serikali yake inapanga kuisadia Korea Kaskazini katika miradi yake ya setalaiti.

Rais wa Urusi, Vladimir Putin na kiongozi wa Korea kaskazini, Kim Jong Un wafanya mazungumzo


Katika ziara hiyo Kim Jong Un amefuatana na maafisa wake wa kijeshi wa ngazi za juu akiwemo afisa wa cheo cha juu kabisa cha Marshal, katika jeshi la ulinzi la Korea Kaskazini, Pak Jong Chon pamoja na mkurugenzi wa idara ya sekta ya utengenezaji risasi, Jo Chun Ryong.

Wakati kiongozi huyo wa Korea Kaskazini akiwa Urusi, nchi yake imefanya majaribio ya  makombora mawili ya masafa marefu, kwa mujibu wa jeshi la Korea Kusini.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW