1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya kuviondoa vikosi vya jeshi Somalia

5 Machi 2020

Kenya inatarajia katika siku kadhaa zijazo kuanza mjadala wa kuondosha vikosi vyake katika mpango wa amani wa Umoja wa Afrika nchini Somalia (Amisom). Jeshi la Kenya limekuwa likihudumu nchini Somalia kwa miaka 8.

https://p.dw.com/p/3Ytrn
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya
Picha: AFP/T. Karumba

MMT_J2 05.03.2020 President Kenyatta Warns Somalia over Incursion - MP3-Stereo

Hatua hiyo inatarajiwa kuchukuliwa baada ya rais Uhuru Kenyatta kutoa tamko la onyo kali saa chache zilizopita dhidi ya Somalia kuhusu kile alichokiita uingiliaji wa mamlaka ya maeneo ya nchi yake.

Hatua hiyo itakuwa ni kukifikisha mwisho kipindi cha takribani miaka minane ya uvamizi uliofanywa na  jeshi la Kenya KDF kwa lengo la kukabiliana na kundi la al-shabaab nchini Somalia.

Katika kile kinacholezwa kutokea Jumatatu iliyopita, serikali ya Kenya imesema jeshi la Somalia lilivuka mpaka na kuharibu mali za Wakenya katika mji wa Mandera, ambao upo mpakani na Somalia.

Hata hivyo waziri wa habari wa Somalia hakuweza kupatikana mara moja kujibu malalamiko ya Kenya.