1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

Karibu wagombea 200 wa bunge nchini Ufaransa wajiengua

2 Julai 2024

Wagombea wasiopungua 200 kutoka vyama mbalimbali wamejiondoa kwenye kinyang'anyiro hicho wakati Ufaransa ikijiandaa na duru ya pili ya uchaguzi wa bunge.

https://p.dw.com/p/4hmZh
Uchaguzi wa bunge nchini Ufaransa
Mgombea wa chama cha mrengo mkali wa kulia nchini Ufaransa cha National Rally Marine Le Pen akiondoka kwenye kituo cha kupigia kura katika duru ya kwanza ya uchaguzi wa bunge, Juni 30, 2024.Picha: FRANCOIS LO PRESTI/AFP

Takwimu hizi zimetolewa na shirika la habari la Ufaransa, AFP.

Muungano wa vyama vya mrengo wa kushoto wa Rais Emmanuel Macron unajaribu kukizuia chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha National Rally kuchukua madaraka.

Mahasimu hao wa kisiasa wanatumai kwamba kujiondoa huko kwa kimkakati kuelekea duru ya pili ya uchaguzi itakayofanyika Jumapili ijayo, kutakizuwia chama cha National Rally kinachoongozwa na Marine Le Pen kupata wingi wa kutosha wa viti 289 kati ya jumla ya viti 577 katika bunge la taifa.

Chama hicho kilishinda duru ya kwanza ya uchaguzi huo iliyofanyika Jumapili iliyopita kwa kupata zaidi ya kura milioni 10.6 na kuibua hofu kwamba huenda kikachukuwa madaraka kwa mara ya kwanza katika historia ya Ufaransa.