1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Scholz aahidi asilimia 2% ya pato jumla kutumika kijeshi

10 Novemba 2023

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz amewaahidi wakuu wa jeshi wa nchi yake kwamba ataitengea sekta ya ulinzi fedha zaidi kwa mpango wa muda mrefu.

https://p.dw.com/p/4YgJ5
Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz
Kansela wa Ujerumani Olaf ScholzPicha: Bernd von Jutrczenka/dpa/picture alliance

Scholz aliahidi kwamba asilimia mbili ya mapato jumla ya nchi, daima itaelekezwa kwenye ulinzi katika kipindi kilichosalia cha miaka ya 2020 na baadaye miaka ya 2030.

Asilimia 2 ya pato jumla ya nchi ni kiwango ambacho kimewekwa na jumuiya ya kijeshi ya NATO kwa kila nchi mwanachama. Ili Ujerumani kufikia kiwango hicho, italazimika kutumia zaidi ya euro bilioni 20 kwa ulinzi kila mwaka.

Scholz: Ujerumani kuwekeza zaidi katika sekta ya ulinzi

Wakati wa mkutano na wanajeshi uliofanyika leo, Scholz amesema hazina maalum ya euro bilioni 100 ya Jeshi la Ujerumani ni hatua ya kwanza muhimu.

Alikuwa akizungumzia hazina maalum ya serikali iliyoanzishwa kwa ajili ya kuboresha jeshi kufuatia uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.