1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KABUL.Wanajeshi wanne wa NATO wauwawa

18 Septemba 2006
https://p.dw.com/p/CDBE

Mlipuaji wa kujitoa muhanga nchini Afghanistan amewauwa wanajeshi wanne wa NATO na watu wengine kadhaa.

Shambulio hilo limetokea kusini mwa jimbo la Kandahar ambako wanajeshi wa Kanada walikuwa katika zoezi la kugawa kalamu na madaftari kwa watoto.

Maafisa wa Nato wamefahamisha kuwa mtu huyo aliiendesha pikipiki yake katikati ya wanajeshi wa NATO na kisha kujilipua.

Shambulio hilo limetokea siku mbili tu tangu makamanda wa NATO walipotangaza kuwa wamekamilisha zoezi la wiki mbili dhidi ya wapiganaji wa Taliban huko kusini mwa Afghanistan.