Sheria na HakiAmerika ya Kaskazini
Trump bado anakabiliwa na kisiki kugombea urais Marekani
29 Desemba 2023Matangazo
Maine limekuwa jimbo la pili kuchukua uamuzi kama huo, kufuatia jukumu la Trump katika tukio la uvamizi wa makao makuu ya Bunge la Marekani mnamo Januari 6, 2021 uliofanywa na wafuasi wake mjini Washington.
Mwezi huu, Mahakama Kuu ya Jimbo la Colorado ilitoa uamuzi wakumzuia Trump kuwania tena urais, hatua ambazo bila shaka zitapingwa katika Mahakama ya Juu ya Marekani.
Soma pia:Mahakama ya juu Michigan yakataa jaribio la kumuondoa Trump
Maamuzi ya majimbo yote mawili yametumia kifungu cha 14 cha Katiba ya Marekani, ambacho kinamzuia mtu aliyehusika na uasi kuwania Urais.