Pande hasimu Sudan zimeahidi kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano kwa siku tatu yaliyofikiwa chini ya usimamizi wa Marekani na Saudi Arabia. Makubaliano hayo yaliyoanza kufanya kazi usiku wa kumkia leo yalitanguliwa na mengine ambayo hayakuheshimiwa tangu kuanza kwa mapigano ya kuwania madaraka nchini Sudan Aprili 15. Rashid Chilumba amezungumza na Abdulfattah Mussa akiwa mjini Tehran.