1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaNiger

Jaribio la mapinduzi linaendelea nchini Niger

26 Julai 2023

Jaribio la mapinduzi linaendelea nchini Niger ambapo rais Mohamed Bazoum anazuwiliwa na askari wa kikosi chake cha ulinzi, ambao wamepewa muda wa mwisho na jeshi kuachana na njama hiyo.

https://p.dw.com/p/4UQcX
Rais wa Niger Mohamed Bazoum
Rais wa Niger Mohamed Bazoum Picha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

Jumuiya ya kiuchumi ya mataifa ya Afrika Magharibi, ECOWAS, Umoja wa Afrika na Umoja wa Ulaya zimelaani kile zilichokiita jaribio la Mapinduzi, maelezo ambayo yametumiwa pia na chanzo kilichoko karibu na Bazoum, kikibashiri kuwa jaribio hilo litafeli. Kikosi cha ulinzi wa rais leo asubuhi kilizuwia njia ya kuingia kwenye makazi ya rais na ofisi yake, na baada ya mazungumzo kushindikana, walikataa kumuachia rais, kimesema chanzo kingine.

Jeshi lasema liko tayari kushambulia

Chanzo hicho kimesema jeshi limewapa wanajeshi hao muda, na kusema liko tayari kuwashambulia ikiwa hawatatii. Bazoum ambaye ni mshirika wa karibu wa Ufaransa, alichaguliwa mwaka 2022, na kuchukua mamlaka katika taifa hilo linalokabiliwa na umaskini mkubwa na lenye historia ya kukosa utulivu.