1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBahrain

Israel, nchi za kiarabu wajadili usalama Abu Dhabi

11 Januari 2023

Israel imeshiriki mojawapo ya mikutano mikubwa na nchi za Kiarabu katika miongo kadhaa wakati wa kongamano lililofanyika katika Umoja wa Falme za Kiarabu.

https://p.dw.com/p/4M0P8
VAE Abu Dhabi Treffen  Vertreter arabische Staaten Israel und USA
Picha: UAE's Ministry of Foreign Affair/AFP

Wajumbe kutoka Bahrain, Misri, Israel, Morocco, Umoja wa Falme za Kiarabu na Marekani walijadiliana njia za kuimarisha ushrikiano wa usalama kupitia ubadilishanaji wa taarifa kama sehemu ya kile kinachoitwa Kongamano la Negev, mkutano ulioanza baada ya kusainiwa mikataba ya kurejesha uhusiano wa kawaida kati ya nchi za Kiarabu na Israel.

Afisa wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani Derek Chollet ameyaeleza mazungumzo hayo ya siku mbili yaliyoanza Jumatatu Abu Dhabi kuwa mkutano mkubwa kati ya Israel na washirika wake wa Mashariki ya Kati, tangu kongamano la amani la Madrid mnamo mwaka 1991.