1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Islamic Jihad watangaza kusitisha mashambulizi Gaza

3 Mei 2023

Kundi la wanamgambo wa Palestina, Islamic Jihad, limetangaza kusitisha mapigano Gaza baada ya wapiganaji wake kurushiana risasi na Israel kutokana na kifo cha mfungwa wa Kipalestina katika gereza la Israel

https://p.dw.com/p/4QpTf
Trauer um Khader Adnan, einem palästinensischen Gefangenen, der im israelischen Gefängnis starb
Picha: Majdi Mohammed/AP

Wapatanishi kutoka Qatar, Misri na Umoja wa Mataifa waliingilia kati kurejesha utulivu kuanzia majira ya saa 10 alfajiri kwa saa za Mashariki ya Kati. Msemaji wa Islamic Jihad, Tariq Salmi amesema awamu moja ya mapambano imemalizika, lakini maandamano ya upinzani yataendelea.

Salmi amesema wapiganaji wao jasiri wameonesha uaminifu na kujitolea kuwatetea watu wao. Khader Adnan aliyegoma kula kwa takribani miezi mitatu alifariki jana akiwa chini ya ulinzi wa Israel.

Kiongozi wa kundi la Hamas, Ismail Haniyeh ameitaka Israel kuurejesha mwili wa Adnan kwa familia yake.