1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Idadi ya waliokufa katika machafuko Bangladesh yafikia 105

20 Julai 2024

Jumla ya watu 105 wameuwawa nchini Bangladesh huku polisi wakipambana bila ukomo dhidi ya maandamano yanayoongozwa na wanafunzi kupinga nafasi za kazi za serikali licha ya marufuku ya mamlaka ya kushiriki mikusanyiko.

https://p.dw.com/p/4iWqO
Kolkata India 2024 | Mwanafunzi wa kikundi cha waandamanaji wakiandamana huko Bangladesh
Wanafunzi wanaoandamana nchini Bangladesh na kudai haki kwa mauaji ya waandamanaji zaidi ya 30 na vikosi vya polisi.Picha: Subrata Goswami/DW

Mapema Ijumaa, mawasiliano ya simu pia yakatwa na idhaa za habari za televisheni hakuwa hewani. Lakini pia mamlka ilikata baadhi ya huduma za simu za mkononi siku iliyopita ili kujaribu kuzima machafuko.

Lakini pia baadae siku hiyo hiyo wanafunzi waandamanaj walivamiagereza moja na kuwaachilia mamia ya wafungwa wakati polisi wakijitahidi kutuliza machafuko, na mikutano mikubwa.