1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ICJ kujadili ukaliaji wa Israel kwenye maeneo ya Palestina

19 Februari 2024

Mahakama ya Haki ya Kimataifa, ICJ, imeanza hivi leo kujadili ombi la Baraza Kuu la Umoja huo kuhusu uhalali wa Israel kuikalia kimabavu ardhi ya Palestina kwa muda wa miaka 57.

https://p.dw.com/p/4cZ25
Uholanzi | Majaji katika mahakama ya Kimataifa ya haki ICJ
Majaji katika mahakama ya Kimataifa ya haki ICJPicha: Piroschka van de Wouw/REUTERS

Kwa muda wa siku 6, majaji 15 wa Mahakama hiyo wataujadili mzozo huo wa miongo kadhaa, na vikao hivyo vinatarajiwa kuhudhuriwa na mataifa mbalimbali. Wawakilishi wa Palestina wamewasilisha hoja zao kuhusu uharamu wa ukaliaji huo.

Licha ya kuwa vita vinaendelea katika Ukanda wa Gaza, vikao vya Mahakama hiyo vinajikita zaidi kuhusu ukaliaji wa kimabavu wa Israel katika maeneo ya Ukingo wa Magharibi, Gaza na Jerusalem Mashariki. 

Soma pia:Mahakama ya ICJ yaitupilia mbali kwa sehemu kubwa kesi ya Ukraine dhidi ya Urusi

Hayo yanajiri wakati Misri ikisema imewasilisha shauri lake ICJ, ikiishutumu Israel kwa matendo haramu katika maeneo ya Palestina na kwamba itatetea hoja yake mbele ya Mahakama hiyo ifikapo Februari 21. 

Diaa Rashwan, mkuu wa kitaifa wa sekta ya habari nchini Misri amesema shauri hilo linapinga vikali sera za Israel za mateso, ubaguzi wa rangi na matendo mengine ambayo yanakiuka waziwazi kanuni na sheria za kimataifa za kibinadamu.