1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

HAMBURG :Miaka 40 ya uhusiano baina ya Ujerumani na Israel

12 Mei 2005
https://p.dw.com/p/CFEM


Rais Horst Köhler wa Ujerumani amesifu mahusiano ya kirafiki na mfungamano uliopo baina ya Ujerumani na Israel.

Rais Köhler amesema hayo katika maadhimisho ya mwaka wa 40 tokea nchi mbili hizo zianzishe mahusiano ya kibalozi baina yao.

Bwana Köhler amesema katika makala ya gazeti aliyoandika kwa ajili ya maadhimisho hayo kwamba Ujerumani na Israel zimethibiti kuwa nchi rafiki zinaoweza kuaminiana.

.