Hali ni tete Burundi huku uchaguzi wa rais ukikaribia
16 Juni 2010Matangazo
Huko nchini Burundi, kuna taarifa kuwa wafuasi wa chama kikuu cha upinzani cha FNL, wameizingira nyumba ya kiongozi wao Agathon Rwasa kwa nia ya kuzuia jaribio linalosemekena ni la serikali kutaka kumkamata kiongozi huyo. Bwana Rwasa ni miongoni mwa viongozi wa upinzani waliotangaza kuususia uchaguzi mkuu ujayo wa urais nchini Burundi.
Polisi ilifiatuwa hata risasi kuwatawanya raia hao na kumuokoa mmoja wao aliyekuwa kavamiwa na umati wa watu wafuasi wa chama cha FNL. Agathon Rwasa amesema haelewi sababu za kutaka akamatwe. Mwanasheria mkuu amesema hakuna waranti waliosaini wa kutaka akamatwe.
Kutoka Bujumbura mwandishi wetu Hamida Issa ametutumia taarifa ifuatayo.
Mwandishi:Hamida Issa
Mhariri: Josephat Charo