1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Guterres azirai nchi kuziba ufa katika mapambano ya ugaidi

Saleh Mwanamilongo
20 Juni 2023

Wafadhili waliohudhuria kongamano lililoitishwa na Umoja wa Mataifa kuisaidia Sudan ameahidi mchango wa kiasi dola bilioni 1.5.

https://p.dw.com/p/4SnhD
Raia wa Sudan wahitaji misaada ya kiutu
Raia wa Sudan wahitaji misaada ya kiutuPicha: AP/picture alliance

Tangazo la ahadi hiyo lilitolewa na mkuu wa misaada ya kiutu wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths mwishoni mwa kongamano hilo la siku moja lililofanyika mjini Geneva. Griffiths aliwakumbusha wafadhili kwamba licha ya michango iliyotangazwa, mzozo wa Sudan bado utaendelea kuhitaji fedha kwa kipindi cha muda mrefu.

Kwa upande mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia  wakimbizi UNHCR Filippo Grandi amewarai wote waliotoa ahadi za michango kuitoa haraka iwezekanavyo kwa sababu tayari shughuli za kiutu nchini Sudan zinakabiliwa na ukata wa fedha.

Mkutano huo wa Geneva ulifanyika katikati ya utekelezaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano kwa siku tatu yaliyoafikiwa na pande hasimu nchini Sudan.