1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MichezoUturuki

Ghana yamuaga Atsu aliyefariki kwenye tetemeko

17 Machi 2023

Waghana walikusanyika leo nje ya jengo la bunge la nchi hiyo mjii Accra kwa ibada ya mazishi ya winga wa timu ya taifa Christiano Atsu, aliyefariki wakati wa tetemeko la ardhi kusini mwa Uturuki mwezi uliopita.

https://p.dw.com/p/4Oqbh
Schweigeminute für Erdbebenopfer Christian Atsu
Picha: Kirsty Wigglesworth/AP/picture alliance

Waombolezaji nchini humo walionekana kupanga mstari ili kumuaga mwanasoka huyo, Atsu ambaye jeneza lake lilikuwa limefungwa bendera ya taifa la Ghana. Atsu ambaye alikuwa na umri wa miaka 31 aliripotiwa kutojulikana aliko baada ya tetemeko la ardhi la Februari 6 kufuatia kuporomoka kwa jengo alimokuwa anaishi katika mji wa Hatay. Mwili wake ulipatikana kwenye vifusi na kusafirishwa hadi nchini Ghana.