GAZA: Jengo la Umoja wa Mataifa lavamiwa
31 Julai 2006Matangazo
Wapalestina siku ya Jumapili,walivamia uwanja wa Umoja wa Mataifa wakati wa maandamano ya kupinga mashambulio ya angani ya Israel yaliyoua raia katika kijiji cha Qana nchini Lebanon.Maafisa wa usalama walifyatua risasi hewani kuutawanya umati huo.Waandamanaji walivunja madirisha ya jengo la UNESCO kwa kurusha mawe baada ya kuandamana katika mji wa Gaza.