1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

G7 kutangaza marufuku kwa almasi ya Urusi

6 Desemba 2023

Viongozi wa kundi la nchi saba tajiri duniani, G7, wanatarajiwa kutangaza marufuku dhidi ya almasi za Urusi na hatua za kusimamia karibu euro bilioni 300 za Benki Kuu ya Urusi ambazo ni mali za nchi hiyo wanazoziulia.

https://p.dw.com/p/4ZqhV
Mawaziri wa Mambo wa Nje wa mataifa ya G7 walipokutana nchini Japan mwezi Novemba 2023.
Mawaziri wa Mambo wa Nje wa mataifa ya G7 walipokutana nchini Japan mwezi Novemba 2023.Picha: Tomohiro Ohsumi/AP Photo

Mkutano huo wa kilele wa viongozi wa G7 unaofanyika kwa njia ya video pia utajadili kuhusu ukomo wa bei ya mafuta.

Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine anatarajiwa kuhudhuria sehemu ya kwanza ya mkutano huo utakaoongozwa na Waziri Mkuu wa Japan Fumio Kishida.

Soma zaidi: Marekani, washirika wazidisha shinikizo la kiuchumi kwa Urusi

Ikiwa karibu miaka miwili baada ya uvamizi wa Urusi, dalili zinaongezeka kuwa uungaji mkono wa Ukraine kutoka kwa Magharibi unapungua wakati ambapo mapambano ya jeshi la Urusi yakionekana kuyumba, na wakati mapato ya mafuta ya Rais Vladmir Putin yakiimarika.

Zelensky jana alifanya uamuzi wa ghafla wa kutohudhuria mkutano mwengine wa vidio hapo jana na maseneta wa Marekani.

Bunge la Marekani limegawanyika zaidi kuhusu uungaji mkono wa Ukraine kuliko ilivyokuwa wakati mwingine wowote katika vita hivyo, huku nchi hiyo ikionekana kuumaliza haraka msaada wa kujeshi uliotolewa na Marekani mpaka sasa.