EU yaishutumu Israel
28 Septemba 2010Matangazo
Rais wa Mamlaka ya Palestina Mahamoud Abbas hapo kabla alitishia kujitoa kwenye mazungumzo ya amani iwapo Israel ingechukua hatua hiyo.
Lakini amewaambia waandishi wa habari katika mkutano wake na Rais Nicolas Sarkozy mjini Paris, kuwa huenda akahirisha uamuzi wa kujitoa au kuendelea na mazungumzo na Israel, baada ya kukutana na wanadiplomasia wa nchi za kiarabu tarehe 4 mwezi ujayo.
Lakini msemaji wa Bwana Abbas,Nabil Abu Rudeina amesisitiza umuhimu wa kusitishwa kwa ujenzi wa makaazi hayo.
Kwa upande wake Rais Sarkozy amesema atawaalika mjini Paris kwa mazungumzo ya amani Rais Abbas, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na Rais Hosni Mubark wa Misri.
Mwandishi:Aboubakary Liongo
Mhariri:Josephat Charo