1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Erdogan: Mkataba wa nafaka kufufuliwa karibuni

Josephat Charo
5 Septemba 2023

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameelezea matumaini yake kwamba mkataba wa nafaka utafufuliwa hivi karibuni. Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema jhautafufuliwa mpaka nchi za Magharibi zitimize masharti yake.

https://p.dw.com/p/4VxNw
Russland Sotschi Türkei Erdogan Putin
Picha: Sergei Guneev/Sputnik/REUTERS

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema itawezekana katika siku chache zijazo kuufufua mkataba wa nafaka ambao Umoja wa Mataifa unasema ulisaidia kupunguza mgogoro wa chakula kwa kufikisha nafaka ya Ukraine katika soko la dunia. Erdogan ameyasema hayo baada ya kukutana ana kwa na kwa mara ya kwanza tangu 2022 na rais wa Urusi Vladimir Putin katika mji wa mapumziko wa Sochi katika bahari Nyeusi.

Putin alisema mkataba huo hautafufuliwa mpaka nchi za Magharibi zitakapotimiza masharti ya Urusi kuhusu mauzo ya nje ya bidhaa zake za kilimo. Erdogan amesema matarajio ya Urusi yanafahamika na wote na kwamba mapungufu yanatakiwa yatatuliwe. Pia amesema Uturuki na Umoja wa Mataifa wameandaa mapendekezo kadhaa mapya kupunguza wasiwasi wa Urusi.

Erdogan ameitaka Ukraine ilegeze msimamo wake dhidi ya Urusi katika mazungumzo kuhusu kuufufua mkataba wa nafaka na isafirishe nafaka zaidi barani Afrika badala ya Ulaya.