1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Dhoruba kali yaupiga mji wa Houston na kuwaua watu wanne

17 Mei 2024

Watu wanne wameripotiwa kufariki kufuatia dhoruba iliyosababisha pia uharibifu mkubwa wa majengo na miundombinu kadhaa huko Houston, Marekani.

https://p.dw.com/p/4fxtM
California 2023
Dhoruba katika mji wa California 2023Picha: Nic Coury/AFP

Watu wanne wameripotiwa kufariki kufuatia dhoruba iliyosababisha pia uharibifu mkubwa wa majengo na miundombinu kadhaa huko Houston, Marekani ambapo pia kaya zaidi ya laki 900,000 zimekosa umeme. Eneo la kusini-mashariki mwa Texas linashuhudia hali hii kwa mara ya pili mnamo mwezi huu.

Soma: Dhoruba kali yapiga maeneo ya Marekani

Mamlaka ya hali ya hewa ya Houston ilitoa tahadhari kuhusu uwezekano wa kushuhudia katika kaunti kadhaa mvua kubwa na upepo mkali. Mamlaka ya jiji hilo imewataka raia kusalia majumbani mwao hasa kutokana na kwamba barabara nyingi hazipitiki huku safari za ndege zikisitishwa kwa muda.

Pia, shule kadhaa huko Houston zimelazimika kufungwa leo Ijumaa kutokana na hali hiyo.