Dawa zakaribia kumalizika Sudan
4 Oktoba 2021Matangazo
Wanachama wa kabila la Beja mashariki mwa Sudan wamezuwia barabara na kulazimisha bandari za Bahari ya Sham kufunga katika wiki za karibuni, kupinga kile wanachosema ukosefu wa mamlaka ya kisiasa katika eneo hilo, pamoja na hali duni ya kiuchumi.
Baraza la mawaziri lilikiri kuhusu madai ya haki ya eneo hilo, na kusisitiza haki ya kuandamana kwa amani:
Hata hivyo, lilionya kuwa kufungwa kwa bandari ya Sudan na barabara kuu zinazounganisha upande wa mashariki na maeneo mengine ya nchi kulikuwa kunaumiza maslahi ya Wasudan wote.