1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

David Cameron ateuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya nje Uingereza

13 Novemba 2023

Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza David Cameron ameteuliwa kuwa Waziri mpya wa Mambo ya Nje akichukua nafasi ya James Clevery ambaye sasa ni Waziri wa Mambo ya Ndani.

https://p.dw.com/p/4YkPr
Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza David Cameron
Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza David Cameron Picha: Suzanne Plunkett/REUTERS

Cameron pia anatarajiwa kuteuliwa kuwa mjumbe wa Baraza la juu la Bunge la Uingereza.

Cameron ambaye uteuzi wake umewashangaza wengi, alikuwa Waziri Mkuu kutoka chama tawala cha Conservative kati ya mwaka 2010 hadi 2016 alipojiuzulu baada ya kura aliyoishinikiza ya maoni ya Brexit ya mwaka 2016, kuibua ukosoaji mkali.   

Waziri Mkuu wa Uingereza Rishi Sunak amfuta kazi Waziri wa Mambo ya Ndani baada ya kukosoa utendaji wa polisi

Mabadiliko haya yanafanyika baada ya Waziri Mkuu Rishi Sunak kumfukuza Waziri wa Mambo ya Ndani Suella Braveman baada ya kukosoa namna jeshi la polisi linavyoshughulikia maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina.

Huku hayo yakiendelea Waziri wa Mazingira Therese Coffey naye amejiuzulu.