1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Cologne yaiaga Bundesliga

30 Aprili 2018

Walikuwa wameshazikwa tayari, lakini msururu wa ghafla wa matokeo mazuri umewapa Hamburg matumaini ya kweli ya kuponyoka tena kaburi la kushushwa ngazi

https://p.dw.com/p/2wvYO
Fußball 1. Bundesliga | Abstieg des 1. FC Köln
Picha: Reuters/K. Pfaffenbach

Baada ya kushinda mechi mbili tu kuanzia mwishoni mwa Agosti hadi mapema Aprili, Hamburg wameshinda tatu kati ya mechi zao nne za mwisho na kuwaweka katika nafasi nzuri ya kuepuka kushushwa ngazi. Ushindi wao wa 3-1 Jumamosi unaweka pointi mbili nyuma ya wapinzani wao Wolfsburg ambao wanashikilia nafasi ya mechi ya mchujo ambayo walimaliza msimu uliopita.

Fußball 1. Bundesliga | VfL Wolfsburg vs Hamburger SV | Jubel
Hamburg bado wanapambana kubakia BundesligaPicha: Imago/Nordphoto/Ewert

Freiburg hatimaye waligonga msumari wa mwisho kwenye jeneza la Cologne na kuwatimua katika Bundesliga baada ya ushindi wa 3-2. Lakini ushindi wa kushangaza wa wikiendi ulikuwa wa Mainz kuwapa RB Leipzig kipigo cha tatu bila hapo jana. Sandro Scwarz ni kocha wa Mainz "ulikuwa ushindi mkubwa na muhimu sana kwetu. Lakini licha ya kila kitu, bado hatujaponea mpaka sasa. jinsi tulivyocheza tulizidiwa nguvu katika kipindi cha pili. kulikuwa na mapambano katika kipindi cha kwanza na matukio ambayo bahati ilikuwa upande wetu. Ni mwanzoni tu ambapo tulipoteza mpira mara kadhaa. lakini uwanja ulikuwa wa kushangaza, mashabiki, kelele, mazingira na hisia. Na kisha tukapata matokeo yanayostahili".

Kileleni mwa msimamo wa ligi, Bayern Munich, iliyofanyiwa mabadiliko makubwa iliibumburusha Eintracht Frankfurt mabao manne kwa moja. Ni mchuano ulioonekana kuwa kionjo tu cha fainali ya kombe la Shirikisho la Ujerumani mnamo Mei 19 mjini Berlin kati ya timu hizo mbili.

Schalke walitoka sare ya 1-1 na Borussia Moenchegladbach na kuendelea kuyashikilia matumaini yao ya kucheza Champions League msimu ujao.

Lakini watamshukuru kipa wa Werder Bremen aliyefanya kazi kweli kweli langoni na kuhakikisha kuwa timu yake inatoka sare ya bao moja kwa moja na Dortmund. Hivyo BVB walioshindwa kuwapokonya Schalke nafasi ya pili.

Mwandishi: Bruce Amani/DPA/Reuters
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman