1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

China yapiga marufuku uingizwaji bidhaa za bahari za Japan

24 Agosti 2023

China imepiga marufuku Alhamis uingizwaji wa bidhaa za baharini kutoka Japan, kwa kile ilichotaja kama hatua ya "ubinafsi" ya Japan ya kutiririsha maji machafu yaliyokuwa kwenye kinu cha nyuklia cha Fukushima.

https://p.dw.com/p/4VXKZ
Japan leitet Fukushima-Wasser ins Meer
Picha: Kim Kyung-Hoon/Reuters

Japan ilianza kuyatiririsha maji hayo yaliyosafishwa na kuondolewa viambata vya mionzi kutoka kinu hicho cha nyuklia cha Fukushima kilichoharibiwa na tetemeko kubwa la ardhi na kuelekea kwenye Bahari ya Pasifiki, katika operesheni ambayo inasisitiza ni salama.

Wizara ya mambo ya nje ya China imeitaja hatua hiyo kama ni ya "kibinafsi na ya kutowajibika" na kusema inaweza ikachochea hatari ya usalama wa chakula kote ulimwenguni kutokana na uchafuzi wa mionzi kwenye chakula.