1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Chama cha Khan chatakiwa kutafuta uongozi mpya

24 Novemba 2023

Tume ya uchaguzi Pakistan imekiagiza chama cha waziri mkuu wa zamani aliyeko jela, Imran Khan kiitishe uchaguzi wa kutafuta uongozi mpya ili kufanikishe ushiriki wake katika uchaguzi mkuu ujao.

https://p.dw.com/p/4ZN10
Pakistan Islamabad Anwaltsteam von Ex-Premier Imran Khan
Mwanasheria wa Waziri Mkuu wa Zamani wa Pakistan Imram Khan, Naeem Haider PanjuthaPicha: AFP

Tume hiyo ya uchaguzi imetowa muda wa siku 20 kwa chama cha Tahreek el-Insaf  kufanya uchaguzi wake wa ndani ili kupata uhalali wa kuendelea kushikilia nembo ya chama chake kwenye uchaguzi huo wa mwakani. Kwa mujibu wa data za Benki ya dunia nembo au alama za vyama katika uchaguzi ni muhimu katika nchi  ambayo idadi ya watu wazima wanaojuwa kusoma na kuandika  ni asilimia isiyozidi 58. Tume imesema ikiwa chama hicho kitashindwa kufuata maagizo hayo, kitapoteza uhalali wa kushikilia nembo yake. Imran Khan amefungwa tangu mwezi  Agosti na hivi sasa anashikiliwa rumande akisubiri kusikilizwa kesi chungunzima zinazomkabili ikiwemo ya madai ya kuvujisha siri za nchi.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW