1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BUSH NA MKUTANO WA NATO

22 Februari 2005
https://p.dw.com/p/CFbs

BRUSSELS:

Rais George Bush wa Marekani amewasili leo katika makao makuu ya NATO-shirika la ulinzi la magharibi mjini Brussels kwa mkutano wa kilele na wanachma 26 wa jumuiya hiyo.Mkutano wake wa kwanza ulipangwa na rais wa Ukrain,Viktor Yuschchenko.Baadae atakua na mkutano na Umoja wa Ulaya uliogawika juu ya uvamizi wa Marekani nchini Irak.

Awali, rais Bush alifungua kinywa kwa chai ya asubuhi na waziri mkuu wa Uingereza ,Tony Blair.Baadae Bw.Blair alisema njia ya kuleta ufumbuzi wa amani wa mgogoro wa Mashariki ya kati sasa imenyoka na rais Bush atatia mkazo zaidi.