1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Burundi yapelekea kikosi chake cha kikanda nchini DRC

23 Agosti 2022

Burundi imewapeleka wanajeshi wake katika eneo lenye machafuko Mashariki mwa Congo, ikiwa ni sehemu ya kwanza ya jitihada ya hivi karibuni inayoratibiwa na mataifa ya Afrika Mashariki kukabiliana na machafuko katika huko

https://p.dw.com/p/4FujS
Symbolbild I Soldaten Burundi
Picha: Mohamed Abdiwahab/AFP/Getty Images

Msemaji wa Jeshi la Burundi, Kanali Floribert Biyereke ameliambia shirika la habari la "The Associated Press" kwamba wanajeshi hao wapo nchini humo kwa jukumu rasmi.

Taarifa ya kuwasili kwa wanajeshi hao katika ardhi ya Kongo, pia imethibitishwa na msemaji wa jeshi la taifa Kongo huko Kivu Kusini, Luteni Marc Elongo, ambae amesema wanajukumu la kuyasaka, makundi ya ndani na nje ya taifa hilo yenye kujihami kwa silaha kwa lengo la kufanikisha amani.

Eneo hilo la lenye kupakana na mataifa ya Rwanda na Uganda, lenye hazina kubwa ya madini limekuwa na idadi kubwa ya makundi yenye kujihami kwa silaha.

Chanzo:afp