1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Burhan amani ya Sudan itapatikana kwa mazungumzo

22 Aprili 2023

Kiongozi wa kijeshi nchini Sudan Jenerali Abdel Fattah al-Burhan amesema pande hasimu nchini humo zinapaswa kukaa pamoja kama taifa kutafuta namna ya kurejesha matumaini na maisha ya kawaida.

https://p.dw.com/p/4QRQa
Themenpaket - Sudan
Picha: ASSOCIATED PRESS/picture alliance

Kiongozi wa kijeshi nchini Sudan Jenerali Abdel Fattah al-Burhan amesema  pande hasimu nchini humo zinapaswa kukaa pamoja kama taifa kutafuta namna ya kurejesha matumaini na maisha ya kawaida.Jenerali al-Burhan ameyasema hayo kutpitia kituo cha televisheni cha  Al Arabiya, ikiwa ni takribani wiki moja baada ya mapigano ambayo yamesabisha vifo vya mamia ya watu.Katika taarifa yake hiyo amesikika akisema "Kila mtu anaathirika na vita hivyo." Hadi jana Ijumaa shirika la Afya Ulimwenguni WHO liliripoti kwamba watu 413 wameuwawa na wengine 3,551 kujeruhiwa tangu kuzuka kwa mapigano hayo.