1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAzerbaijan

Azerbaijan yakataa kushiriki mazungumzo ya amani na Armenia

16 Novemba 2023

Azerbaijan imekataa leo kushiriki katika mazungumzo ya kurekebisha mahusiano na hasimu wake mkuu Armenia ambayo yalipangwa kufanyika Marekani mwezi huu.

https://p.dw.com/p/4YtE8
Athari za mapigano kati ya Armenia na Azerbaijan yaliyozuka Septemba 2023.
Azerbaijan na Armenia zimepigana vita mara mbili tangu kuanza kwa mzozo wa kuwania jimbo la Nagorno Karabakh mwanzoni mwa miaka ya 1990.Picha: Aik Arutunyan/SNA/IMAGO/

Azerbaijan imesema Marekani ina msimamo wa upendeleo. Wizara ya mambo ya kigeni ya Azerbaijan imesema haioni kama inawezakana kufanyika mkutano huo unaopendekezwa wa ngazi ya Mawaziri wa Mambo ya Kigeni wa jamhuri hizo mbili za uliokuwa muungano wa Sovieti mjini Washington Novemba 20.

Waziri Mkuu wa Armenia Nikol Pashinyan amesema leo kwamba "nia ya kisiasa ya Yerevan ya kutia saini, katika miezi ijayo, makubaliano ya amani na Azerbaijan bado haitetereki."

Azerbaijan na Armenia zimekuwa kwenye mgogoro wa mipaka uliodumu kwa miongo kadhaa kuhusiana na mkoa wa Azerbaijan wa Nagorno-Karabakh, ambao Baku iliukomboa Septemba mwaka huu baada ya operesheni kali ya kijeshi dhidi ya wanaharakati wa Kiarmenia wanaopigania kujitenga.