1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
AfyaAustralia

Australia: Mama mmoja atolewa mnyoo hai kwenye ubongo wake

29 Agosti 2023

Madaktari nchini Australia wameuondoa mnyoo hai kutoka kwenye ubongo wa mwanamke mwenye umri wa miaka 64.

https://p.dw.com/p/4Vicy
Mnyoo huo alikuwa na urefu wa sentimeta 8.
Mnyoo huo alikuwa na urefu wa sentimeta 8.Picha: AAP/picture alliance

Mnyoo huo alikuwa na urefu wa sentimeta 8.

Aina ya mnyoo huo kwa jina Ophidascaris robertsi unapatikana zaidi kwenye baadhi ya chatu na kwa kawaida huingia katika miili ya viumbe wengine lakini si miili ya binadamu.

Wanasayansi nchini Australia wamechapisha taarifa juu ya mkasa huo usiokuwa na kifani.

Mwanamke aliyetolewa mnyoo huo alikuwa analalamika kusumbuliwa na maumivu kwa muda mrefu.