1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Argentina yabeba Copa America kwa kuibwaga Brazil

12 Julai 2021

Matukio mawili ya ukame wa muda mrefu yalifikia kikomo Jumamosi katika fainali ya Kombe la Amerika Kusini. Argentina ilishinda taji lake la kwanza kuu tangu mwaka wa 1993 baada ya ushindi wa 1 – 0 dhidi ya Brazil

https://p.dw.com/p/3wLYP
Fußball Copa America Finale Argentinien - Brasilien
Picha: Silvia Izquierdo/AP Photo/picture alliance

Na Lionel Messi hatimaye alinyanyua kombe lake la kwanza kuu akiwa na timu yake ya taifa na kujaza mojawapo ya mapengo makubwa kabisa katika taaluma yake yenye mafanikio makubwa.

Bao la ushindi ls Argentina katika dimba la kihistoria la Maracana mjini Rio de Janeiro lilikuja katika dakika ya 22 kutoka kwa Angel di Maria mwenye umri wa miaka 33.

Na baada ya kipenga cha mwisho kupulizwa, Messi mwenye umri wa miaka 34 alilia machozi ya furaha. Baada ya kupoteza mara nne katika fainali, kuondolewa mapema katika mashindano makubwa na hata uamuzi wa kustaafu soka la timu ya taifa, nyota huyo alisherehekea kwa aina yake. Messi alikuwa na umri wa miaka 6 wakati Argentina ilishinda kombe mara ya mwisho. Katika mashindano haya ya Copa America, ametajwa kuwa mchezaji bora akiwa na mabao manne na asisti tano. Nahodha huyo pia alivunja rekodi ya kuichezea timu ya taifa, mechi 151.

AFP, AP, Reuters, DPA