1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Angola kujiondoka katika mataifa ya OPEC

22 Desemba 2023

Angola imetangaza kuwa inaondoka katika kundi la nchi zinazozalisha mafuta kwa wingi duniani - OPEC. Hatua hiyo inatokana na miito ya kutaka kupunguzwa uzalishaji wa mafuta ili kudumisha bei za juu.

https://p.dw.com/p/4aSwj
Saudi Arabien | Öl-Lager am Hafen von Jubail
Picha: Bilal Qablan/AFP/Getty Images

Waziri wa mafuta wa taifa hilo la Kiafrika Diamantino de Azevedo, amesema Angola haifaidiki na chochote kwa kubaki katika shirika hilo. Nchi hiyo ilijiunga na OPEC katika mwaka wa 2007. Angola inasema sera za OPEC hazitumiki tena kwa maslahi yake ya kuepuka kushuka kwa uzalishaji na kuheshimu kandarasi. Angola na Nigeria, nchi mbili zinazozalisha mafuta kwa wingi katika eneo la kusini mwa jangwa la Sahara, zilipinga uamuzi huo wa OPEC. Nchi hizo zinataka kuendeleza uzalishaji kama chombo cha kupata fedha za kigeni. OPEC, kundi lenye wanachama 13 lililoanzishwa mwaka wa 1960, liliongeza wanachama wapya 10 katika mwaka wa 2016 chini ya jina la OPEC+, katika juhudi ya kutaka nguvu zaidi.